MANCHESTER UNITED NA TOTTENHAM ZAAGA LIGI YA EUROPA

Goli safi la Philippe Coutinho liliweza kuiua Manchester United na kufuta matumaini ya kutinga hatua ya nane bora ya Ligi ya Europa baada ya kutoka sare ya bao 1-1 kwenye mchezo wa jana katika dimba la Old Trafford.

Kikosi cha kocha Jurgen Klopp kilikuwa kinalinda magoli yake mawili kwa bila iliyoyapata kwenye mchezo wa awali Anfield, lakini penati ya dakika 32 iliyopigwa na Anthony Martial lilifufua matumaini kwa United kabla ya Countinho kuharibu mambo.
    Anthony Martial akiwa na wachezaji wenzake wakishangilia baada ya kupiga penati 
             Kipa De Gea na beki Blind wakiwa hoi baada ya Coutinho kufunga bao
 Mshambuliaji Pierre-Emerick Aubameyang alipachika mabao mawili na kuiondoa Tottenham katika ligi ya Europa baada ya Borussia Dortmund kuibuka na ushindi wa mabao 2-1, na hivyo kuwa na mtaji wa mabao 5-1 ikijumuishwa na mchezo wa awali.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa raia wa Gabon, alikuwa azuiliki katika mchezo huo wa jana usiku na kuonyesha kwanini klabu kubwa za Ulaya zinahaha kuinasa saini yake ili aweze kujiunga nazo.
                          Pierre-Emerick Aubameyang akiwachia shuti lililojaa wavuni
You might also like:
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment