CHEKI SEVILLA WALIVYOANGUSHA BONGE LA PATI BAAADA YA KUTWAA TENA UBINGWA WA EUROPA









Sevilla kwa mara nyingine tena wamechukua ubingwa wa EUROPA baada ya kuwatungua Dnipro kwa mabao 3-2 na kuwa klabu ya kwanza barani Ulaya kushinda taji hilo mara nne kwa matokeo yanayofanana yaani magoli 3-2 mara hizo zote. 
 
Wahispania hao mara ya kwanza walichukua miaka ya 2006 and 2007 wakati huo likiitwa Uefa Cup - na sasa wamechukua tena kwa mara ya pili mfululizo huku Carlos Bacca akipiga mbili na kujihakikishia ushujaa wa mchezo.
Wababe hao wa Unai Emery mwaka jana walishinda kwa mikwaju ya penati baada ya mchezo kumalizika kwa are ya  0-0 dhidi ya Benfica, lakini wakati huu wamekataa kabisa kufika huko.
 
Grzegorz Krychowiak aliipatia Sevilla bao la kwanza huku Bacca akiongeza la pili na tatu na kuhitimisha ushindi kwa wababe hao wa EUROPA.
Nao Dnipro ambao wanatokea nchini Ukraine walijipatia magoli yao kupitia kwa nahodha wao Ruslan Rotan na Nikola Kalinic.
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment