Sevilla
kwa mara nyingine tena wamechukua ubingwa wa EUROPA baada ya kuwatungua
Dnipro kwa mabao 3-2 na kuwa klabu ya kwanza barani Ulaya kushinda taji
hilo mara nne kwa matokeo yanayofanana yaani magoli 3-2 mara hizo
zote.
Wahispania
hao mara ya kwanza walichukua miaka ya 2006 and 2007 wakati huo
likiitwa Uefa Cup - na sasa wamechukua tena kwa mara ya pili mfululizo
huku Carlos Bacca akipiga mbili na kujihakikishia ushujaa wa mchezo.
Wababe
hao wa Unai Emery mwaka jana walishinda kwa mikwaju ya penati baada ya
mchezo kumalizika kwa are ya 0-0 dhidi ya Benfica, lakini wakati huu
wamekataa kabisa kufika huko.
Grzegorz
Krychowiak aliipatia Sevilla bao la kwanza huku Bacca akiongeza la pili
na tatu na kuhitimisha ushindi kwa wababe hao wa EUROPA.
0 comments:
Post a Comment