Kocha
wa timu ya soka Sunderland ya England, Dick Advocaat ametangaza kubwaga
manyanga kuendelea kuifundisha klabu hiyo, japokuwa kocha huyo
amefanikiwa kuiokoa timu hiyo kutoka katika janga la kushuka daraja
msimu huu.
Advocaat
alijiunga klabuni hapo mwezi March mwaka huu akiziba pengo la Gus
Poyet, na amesema kuwa hategemei kuendeleza ujuzi wake katika utawala wa
timu hiyo. ''
Sunderland imekuwa ni moja ya sehemu muhimu kwenye fani
yangu. Wakati fulani katika maisha yako wapaswa kufanya uamuzi"
Advocaat.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Sunderland Ellis Short, amesema
kuwa amefadhaishwa na taarifa ya kocha huyo lakini anaheshimu uamuzi
wake huku akiahidi kuendelea kumshukuru.
0 comments:
Post a Comment