
Guardiola ameweka wazi kuhusu wachezaji wake Sergio Aguero, Zabaleta na beki wake wa kati na nahodha wao Vincent Kompany, Guardiola ameweka wazi kuwa Kompany ambaye aliumia goti katika mchezo dhidi ya Crystal Palace uliomalizika kwa ushindi wa 2-1, atakuwa nje kwa wiki nne hadi sita.

“Sergio Aguero hajaumia anatatizo dogo tu katika mguu wake na Zabaleta pia tutajua tukifanya mazoezi leo, lakini Vincent Kompany atakuwa nje ya uwanja kwa wiki nne hadi sita, tuna njia nyingi za kuziba pengo lake lakini Toure pia anaweza kucheza beki wa kati”
0 comments:
Post a Comment