Ikumbukwe mkutano huo umeitishwa siku moja kabla ya mgomo, ambao ulipangwa kufanyika October 18, 2016.
Ijumaa ya wiki iliyopita, Waziri wa ajira nchini Kenya, Phyllis Kandie alituma barua kwa pande zote mbili, pamoja na kuteua kamati ya wajumbe watano kushughulikua mgogoro huo.
Chama cha wafanyakazi nchini Kenya KALPA kimetoa mapendekezo yake ambapo moja ya walichoagiza ni pamoja na kutaka Mkurungenzi Mtendaji wa shirika la ndege Kenya Airways, Mbuvi Ngunze na mwenyekiti Dennis Awito wajiuzulu nafasi zao mara moja.
Serikali ya Kenya imeona madhara ya mgomo uliopangwa kufanywa na Marubani wa shirika la ndege la Kenya Airways, baada ya abiria kukata tiketi za safari zao na kucheleweshwa kwa safari za ndege mwezi uliopita.
October 16, 2016, Kenya Airways ililazimika kukatisha safari zake tano katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta baada ya marubani na wafanyakazi wa shirika hilo kugoma kufika uwanjani
.
.
0 comments:
Post a Comment