Kocha Jose Mourinho ameanza vyema akiwa na Manchester United kwa kutwaa kikombe baada ya Zlatan Ibrahimovic kufunga goli la kichwa la dakika za mwisho na kuibuka na ubingwa wa ngao ya hisani katika dimba la Wembley.
Katika mchezo huo ulioishia kwa magoli 2-1 dhidi ya Leicester City, Jesse Lingard ambaye alifunga goli la ushindi katika kombe la FA, wakiwa na kocha Louis van Gaal, alipachika goli la kwanza baada ya kuwatoka mabeki wanne.
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Uingereza Leicester walijibu mapigo baada ya Marouane Fellain kutoa pasi mbovu ya nyuma iliyompa fursa mshambuliaji hatari Jamie Vardy kuchomoka na kuachia shuti lililomshinda kipa David de Gea.
Jesse Lingard akiachia shuti lililojaa wavuni na kuandika goli la kwanza
Zlatan Ibrahimovic akipiga mpira kwa kichwa ambao ulizaa goli la pili
Zlatan Ibrahimovic akiangalia mpira alioupiga kwa kichwa ukijaa wavuni
0 comments:
Post a Comment