1. Clinton aidhinishwa kuwa mgombea wa Democratic


Bi Hillary Clinton mkewe Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton, amekuwa mwanamke wa kwanza kupeperusha bendera ya chama kikubwa nchini Marekani baada ya kuidhinishwa na chama cha Democratic kuwania nafasi ya urais.
Wajumbe katika mkutano wa kitaifa wa Chama uliofanyika katika mji wa Philadelphia, wamemteua rasmi mwanamke huyo aliyekuwa Seneta na waziri wa mambo ya nje kama mgombea wao wa urais. Dakika chache zilizopita mumewe Bi Clinton alimaliza kulihutubia mkutano huo wa wajumbe.

Katika siku ya mwisho hapo kesho, Rais Barrack Obama na Bi Hillary Clinton watakuwa wazungumzaji wakuu katika mkutano huo wa wajumbe mjini Philadelphia.
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment