CRISTIANO RONALDO AMEFUNGA MAGOLI MAWILI WAKATI URENO IKIUWA

Mshambuliaji Cristiano Ronaldo amefunga magoli mawili wakati Ureno ikiwa na wachezaji 10, ikiifurumushia Estonia mvua ya magoli 7-0, katika mchezo wa wa mwisho wa kujiandaa na michuano ya Euro 2016.

Katika mchezo huo Ricardo Quaresma naye alitigisa nyavu mara mbili, na Danilo, Eder moja kila mmmoja huku Karol Mets akikamilisha kichapo hicho kwa kujifunga.

Mchezo huo ulikuwa wa kwanza kwa Ronaldo kushuka dimbani tangu ashinde Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya mwezi uliopita akiwa na timu yake ya Real Madrid.
               Cristiano Ronaldo akiruka kuupiga mpira kwa kichwa kilichozaa goli
                          Ricardo Quaresma akiachia shuti kati kati ya mabeki wa Estonia
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment