BRAZIL YAJIPIGIA HAITI MAGALI 7 KATIKA MICHUANO YA COPA AMERIKA

Timu ya Taifa ya Brazil imeichakaza Haiti kwa magoli 7-1, wakati Philippe Coutinho akifunga magoli matatu yaani hat-trick katika mchezo wa michuano ya Copa Amerika.

Katika mchezo huo Philippe Coutinho alikuwa wakwanza kuzifumania nyavu, ambapo pia Renato Augusto naye aliifungia Brazil magoli mawili wakati kikosi cha Dunga kikifanya mauaji makubwa.

Mchezaji aliyetokea benchi Gabriel Barbosa na Lucas Lima wote nao waliifungia Brazil na kuifanya Brazil kujikusanyia pointi nne, huku ikiwa na mchezo mmoja wa mwisho katika kundi lao dhidi ya Peru.
                                                    Philippe Coutinho akiachia shuti lililojaa wavuni
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment