JOHN TERRY ASAINI MWAKA MMOJA CHELSEA


Hatimaye nahodha wa matajiri wa jiji la London Chelsea, John Terry amesaini mkataba wa mwaka mmoja zaidi wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo yenye maskani yake darajani ambayo msimu huu haukuwa mzuri kabisa kwao. 

Kulikuwa na hati hati ya nahodha huyo mwenye miaka 35 kipenzi cha mashabiki wa timu hiyo kuondoka mara baaada ya kumalizika msimu wa ligi kuu England 2015/16. 

Mataji aliyotwaa na Chelsea ni pamoja na ligi kuu England (2005, 2006, 2010, 2015), Klabu bingwa Ulaya (2012), Europa League (2013), FA Cup (2000, 2007, 2009, 2010, 2012), League Cup (2005, 2007, 2015), Community Shield (2009) 


Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment