Kundi la wapiganaji wa Kikurdi la
TAK limesema ndilo lililofanya shambulizi baya kubwa katika Jiji Kuu
la Ankara nchini Uturuki.
Taarifa iliyotolewa kwa njia ya
mtandao kundi hilo limesema shambulio hilo lililouwa watu 37 ni la
kulipa kisasi dhidi ya operesheni za kijeshi eneo la Wakurdi la
kusini mashariki.
Wapiganaji wa kundi la TAK, ambao ni
sehemu ya Chama cha Wafanyakazi wa Kikurdi (PKK) kilichopigwa
marufuku, wamesema ndio pia waliohusika na mlipuko wa bomu la Ankara
mwezi uliopita.
0 comments:
Post a Comment