Milioni 9 za Rais Magufuli leo March 24, 2016….ninayo video yenye sekunde 15 hapa

Rais Magufuli ametoa zawadi ya vyakula na vinywaji vyeye jumla ya Shilingi milioni tisa na laki tatu katika vituo vya malezi kwa Wazee na watoto wanaoishi katika mazingira magumu nchini ili kusherekea sikukuu ya pasaka.
Akitoa zawadi hizo kwa niaba ya Rais Magufuli Naibu kamishna wa Ustawi wa jamii Rabikira Mushi alisema..Awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kumshukuru mwenyez Mungu kwa kutujaalia sote kujumuik mahali hapa kwa ajili ya tukio hili muhimu la kukabidhi zawadi za sikukuu kutoka kwa Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli‘ >>> Rabikira Mushi
Aidha shukrani hizi napenda pia zimfikie mheshimiwa Rais  kwa upendo wake wa dhati kabisa na kuona umuhimu wa kushiriki kutoka kusherekea sikukuu ya Pasaka kwa pamoja na watu walio katika makundi maalum wakiwemo watoto walio katika mazingira hataridhi na wazee wanaolelewa katika vituoRabikira Mushi
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment