Huu ndio ugonjwa wa kuambukiza unaosababisha vifo vingi duniani, Tanzania nayo imehusishwa



Kila tarehe 24 March dunia huadhimisha siku ya ugonjwa wa kifua kikuu, Siku hii ni maalum kwa ajili ya kuhamasisha watu kuhusu umuhimu wa kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa huo katika jamii.
Leo March 24 2016 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy  Mwalimu alikutana na waandishi wa habari Dar es salaam na kuelezea kuhusu changamoto za ugonjwa huo.

Kifua kikuu ni ugonjwa unaoambukizwa na bakteria wanaojulikana kwa jina la Mycobacteria tuberculosis, vimelea vyake huenea kwa njia ya hewa na havichagui aina ya mtu pia hutoka kwa mgonjwa ambaye hajaanza matibabu na kuambukiza wengine‘ ;-Ummy Mwalimu
Licha ya kuwa kifua kikuu kinatibika, lakini ndio ugonjwa pekee wa kuambukiza unaosababisha vifo vya watu wengi katika jamii, ambapo watu watatu hufariki kila baada ya dakika moja. Takwimu zinaonyesha Tanzania takribani watu 12,000 hufariki kwa ugonjwa huu‘ ;-Ummy Mwalimu
Natoa wito kwa wananchi wote kuwa na kawaida ya kufanya uchunguzi wa afya zao ili kugundua tatizo mapema na kuzuia kuenea kwa Kifua kikuu, tukifanya hivyo tutapunguza kuenea kwa ugonjwa huu‘ ;-Ummy Mwalimu
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment