KIPIGO CHA JUVE SHEREHE KWA VILABU VYA EPL


Premier League-clubs

Baada ya Juventus kuondoshwa kwenye michuano ya Champions League, mtandao wa ESPN  umeandika kwamba, matokeo hayo ni habari njema kwa vilabu vya England Premier League.

Kipigo cha Juve kinamaanisha vilabu vya Premier League bado vitaendelea kupata nafasi nne kwenye michuano ya vilabu bingwa Ulaya katika msimu ujao 2017-18.


Kufanya vizuri kwa vilabu vya Italy kungepelekea kupoteza nafasi ya EPL kupeleka timu nne kwenye michuano ya Champions League lakini nafasi hiyo wameipoteza kutokana na Juve kuondolewa kwenye hatua ya 16 bora.

Juve kung’olewa na Bayern kuinaicha timu moja ya Serie A kwenye michuano ya Ulaya.

Lazio inaweza kuongeza ‘coefficient points’ hadi kufikia 2.5 endapo itafanikiwa kuchukua Europa League, lakini England hadi sasa tayari inapointi 3.97 mbele ya Italy.

Kama England itapeleka timu tatu pekee kwenye michuano ya Champions League basi ile dhana kwamba the Premier League ni bora duniani haita kuwepo tena.

England imeshindwa kufanya vizuri kwenye michuano ya Champions League kwa kushindwa kupeleka timu timu zaidi ya moja kwenye hatua ya robo fainali lakini pia hali ni tete katika Europa League ambapo Tottenham Hotspur ipo nyuma kwa magoli 3-0 dhidi ya Borussia Dortmund baada ya mchezo wa kwanza.

Timu kutoka Ujerumani na Hispania zimekuwa zikifanya vizuri zaidi ya zile za England msimu huu.

Vilabu vya Serie A vimepata pointi 19.00 msimu uliopita, mara ya kwanza vilivishinda vilabu vya Premier League tangu msimu wa 2005-06.

Vilabu vya italia vilitakiwa kufanya hivyo tena huku vilabu vya England vikiendelea kuboronga ili vinyang’anye nafasi nne ilizonazo England kwenye michuano ya Champions League.

Lakini nafasi ya Italy ilipotea baada ya Sampdoria kupigwa vibaya kwenye raundi ya tatu ya Europa League. Hiyo ikatoa mwanya kwa England ambayo vilabu vyake vya Southampton na West Ham pia vilishindwa kufuzu hatua ya makundi ya michuano hiyohiyo.

Kipigo cha Fiorentina dhidi ya Tottenham kwenye hatua ya 32 bora ya Europa League ilizidi kudidimiza ndoto zao, na kwa sasa hakuna nafasi ya Italy kuipiku England kuingiza vilabu vinne kwenye michuano ya klabu bingwa Ulaya.


Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment