Selemani
Rashidi, naomba msaada kwa yeyote anisaidie niweze kufanyiwa matibabu
kwa kinyama kilicho jitokeza kichwani mwangu toka nilipo zaliwa.
Selemani Rashidi, anapoishi na mama yake mzazi
Selemani
Rashidi (kushoto), akiwa na mama yake mzazi pichani, ambaye alisimulia
mkasa mzima wa mwanaye, alizaliwa akiwa mzima na baada ya kuzaliwa
alipatwa na matatizo ya ugonjwa wa Degedege na alimpeleka kwa mganga wa
kienyeji na kupona matatizo hayo na ndipo kikaota kipele kichwani cheusi
na kikawa kinakuwa na kushikana na sikio, kutokuwa na uwezo wa kipesa
hakuweza mpeleka popote, Baba yake yapata Miaka kumi na tano toka
afariki na ukizingatia ni pesa inayo hitajika, hayo yalisemwa na mama
yake mzazi ambaye anaitwa Zamda Kibosha, wakiwa wamekaa kwao maeneo ya
kitongoji cha Lugongoni, (A) Kataa ya Nguruka Wilaya ya Uvinza Mkoa wa
Kigoma, Mama yake anasema mwanaye baada ya kuota kinyama hicho, kauli
kutoka ni kwa shida, akijibu maramoja harudii tena kuongea na chooni
anakwenda mwenyewe na kula anakula kama kawaida, mama anaomba kwa mtu
yoyote mwenye kuona na kusia anaomba msaada wa hali na mali ili mwanaye
apate matibabu, kwa mawasiliano mwenye chochote kitumwe kwenye namba 0687946492, Mariam Hamza Thabiti, Nguruka kigoma.
(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
0 comments:
Post a Comment