ORLANDO PIRATES YACHUKUA WATANZANIA WATANO, MALINZI ATOA SHUKURANI


Klabu kongwe ya Afrika Kusini, Orlando  Pirates, inatarajiwa kuchukua wachezaji watano chini ya umri wa miaka 15 ambao wanakwenda kwenye majaribio klabuni hapo na iwapo watafaulu, itakuwa tiketi ya kuchukuliwa moja kwa moja.

Vijana hao wanatarajiwa kuondoka nchini Agosti 29, mwaka huu chini ya Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Salum Madadi ambapo mtihani wao wa kwanza utakuwa Septemba 5, kutakuwa na mashindano ya Multichoice nao watashiriki.
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi, ametoa shukrani zake kwa Mwenyekiti wa Pirates, Dk Irvin Khoza ambaye alikuwa mwepesi kukubaliana na ombi lake la kuchukua vijana hao, ikiwa ni sehemu ya kupanua soko la soka la Tanzania.
Wachezaji hao ni Asad Juma kutoka Zanzibar, Issa Abdi na Maziku Amad (Dodoma), Athuman Maulid (Kigoma) na Kelvin Deogratius wa Geita.

Wakati huohuo, jumla ya wachezaji 20 waliochaguliwa kwenye mashindano ya vijana ya taifa yaliyofanyikia Mwanza hivi karibuni, wanatarajiwa kujiunga na Akademi ya Alliance ya Mwanza.
P yhaa tv coming soon

Tuwe Pamoja Huku Ilikupata Stori ZOTE
share
 

face book ipyana stephen



  Share



usisahau kusubscribe YouTube kwa kubonyeza hapa >>>Videos 

Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment