Karibu watu 60 wauawa Nigeria


Ripoti kutoka nchini Nigeria zinasema kuwa karibu watu 60 huenda waliuawa wakati wa shambulizi katika kijiji kimoja kaskazini mashariki mwa nchini lililoendeshwa na watu wanaoshukiwa kuwa wanachama wa na Boko Haram.
Shambulizi hilo lilitokea katika jimbo la Yobe lilifanyika Alhamisi iliyopita na habari hizo zimepatikana kutoka kwa wale walionusurika.
Mwandishi wa BBC nchini Nigeria anasema kuwa ukweli kuwa ilichukua siku tano kabla ya shambulizi hilo kujulikana, ni ishara kuhusu jinsi hali ya usalama ilivyo eneo hilo.
Walioshuhudia walisema kuwa wanamgambo wa Boko Haram waliwasili katika kijiji hicho wakitumia pikipiki ambapo walianza kuwafyatulia watu risasi.
Mikakati ya jeshi Nigeria imelidhoofisha kundi la Boko Haram miezi ya hivi majuzi lakini sehemu zingine za kaskazini mashariki mwa Nigeria kama Yobe na jimbo jirani la Borno yako katika hali mbaya kiusalama.
P yhaa tv come soon

Tuwe Pamoja Huku Ilikupata Stori ZOTE
share
 

face book ipyana stephen



  Share



usisahau kusubscribe YouTube kwa kubonyeza hapa >>>Videos 

Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment