SAFARI YA MATUMAINI YA TANZANIA KUELEKEA FAINALI ZA AFRIKA 2019


Habari wana familia ya mpira wenzangu. Tumeongea mengi na tumesoma mengi kuhusu  kukua kwa mpira wetu Tanzania.
Binafsi naona wanachi wengi tunakosoa kuliko kutoa ushauri wa nini kifanyike. 
Nimekaa nimeona nije na ushauri huu ambao naamini pale nilipoishia kuna Mtanzania mwenzangu atakua na jicho la ziada ataongezea au atapunguza pale nilipozidisha au kupunguza lengo likiwa ni kujenga kuliko kulaumu tu.

{1}.   Ili kuanza kutengeneza msingi imara wa mpira wetu,tuamue kwamba kila timu ya ligi kuu nilazima iwe na timu C ya under 17 na tuweke ligi kuu ya vijana hawa wa under 17 .kama huna timu hii basi unapoteza uhalali wa kucheza ligi kuu.

{2}    kila timu ya ligi kuu ni lazima iwe na timu B yaani under 20 na tuweke ligi kuu ya vijana wa umri huo na tutafute bingwa wake kwa msimu mzima na kama huna timu hii unapoteza uhalali wa kushiriki ligi kuu.

{3}  Mashindano haya ya vijana yasifanyike kama bonanza kuwaita sehemu moja, bali iwe ligi kama ilivyo ligi kuu.
kila timu icheze nyumbani na ugenini na hapa kama timu yako A inayoshiriki ligi kuu itashuka daraja basi na timu zako zote unashuka nazo kwenda kujiunga na daraja la kwanza bila kujali timu yako B au C  ilishika nafasi ya ngapi kwenye ligi TWO au ligi TREE ili kutoa nafasi kwa zile timu zitakazopanda zipate nafasi kwenye timu a,b na c .

{4} Na kwa timu za daraja la kwanza pia kanuni itakua hiyo lazima uwe na timu hizo ndio upate uhalali wa kucheza ligi daraja la kwanza. 
Mimi naamini tukisimamia vizuri na kuwa wakari na lengo moja hapa tutakua tunatengeneza msingi imara wa soka letu na kuepuka lawama hizi tunazotupa kwa viongozi wetu wa TFF na kocha bila kuangalia tumekwama wapi. 
Timu hizi  za vijana sio ziwe kwenye makaratasi tu bali zionekane kweli zipo na jicho letu tulitupie sana huku. 

Naamini haya yakifanyika tutatumia ligi hizi kuvuna vipaji nchi nzima kwa ajili ya timu zetu za Taifa kuanzia ile ya under 17, 19,20 na senior team.

Nchi nyingi zimeendelea duniani kwa kuacha uvivu na kuwekeza kwenye soka la namna hii na mwisho wamefanikiwa.
TAENDELEA KUKUPATIA HABARI,PICHA NA MAELEZO,ENDELEA KUNITEMBELEA HAPA.
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment