T.I anaweza kumpa mkewe talaka kisa Floyd Mayweather?…


Kumekuwa na bifu ya chini kwa chini kati ya rapper T.I na boxer Floyd Mayweather tangu mwaka 2014 ambayo inasemekana ilisababishwa na mke wa T.ITinny kupiga picha na Mayweather na kupost kwenye mtandao wake wa Instagram kitu ambacho T.Ihakupendezwa nacho na kuanza kurushiana maneno na Mayweather.
Headlines za bifu yao zimeibuka tena baada ya Tinny kupost picha kwa mara nyingine akiwa na Maria Carey na Floyd Mayweather ambaye mpaka sasa hayuko kwenye mahusiano mazuri na mumewe huku akisema alialikwa na Maria Carey akaona sio mbaya kupiga picha, maelezo ambayo yanatofautiana na video ambayo imesambaa mitandaoni ikimuonyesha  Mayweather akicheza muziki na Tinny.
Inasemekana pia T.I ana mpango wa kutoa talaka baada ya video hiyo kusambaa mitandaoni kitu ambacho baadhi ya mashabiki wanasema T.I atakuwa hajafanya kitu cha busara kumuacha mkewe kisa amecheza muziki na Mayweather labda kama ana sababu nyingine.
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment