Olimpiki: Venus na Serena Williams nje kwenye ‘women’s doubles tennis’

Katika moja ya matokeo ya kushangaza zaidi kwenye michuano ya Olimpiki inayoendelea jijini Rio, Brazil, watetezi wa medali ya dhahabu Venus na Serena Williams wametolewa kwenye raundi ya kwanza ya mchezo wa tennis wa wanawake wawili wawili.

36FC1C8E00000578-0-image-a-60_1470612988143

Dada hao wa Williams hawajawahi kushindwa kwenye mechi ya aina hiyo kwenye Olimpiki.

36FC2B8E00000578-0-image-a-59_1470612979549

Wabaya wao walikuwa ni Lucie Safarova na Barbora Strycova wa Jamhuri ya Czech waliowashinda kwa seti 6-3 na 6-4.
36FC2F7E00000578-0-image-a-57_1470612680756

Williams walishinda medali za dhahabu mwaka 2000, 2008 na 2012 wakiwa wawili. Kupoteza huko kunakuwa mwisho kwa Venus kwenye mashindano hayo mwaka huu.
36FC423500000578-0-image-a-58_1470612721987
Serena ataendelea na harakati zake za kuitetea medali yake ya dhahabu ya mchezo wa mmoja mmoja. Alishinda mechi yake ya kwanza Jumamosi dhidi ya Daria Gavrilova wa Australia.
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment