NIDA yaahidi kutoa namba za vitambulisho vya uraia milioni 23

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Bi. Rose Mdami ametangaza kuwa mpaka ifikapo Disemba 31 mwaka huu zaidi ya watanzania milioni 23 watakuwa na namba utambulisho wa vitambulisho vya Uraia.


Rose-Mdami-702x336

Bi Rose amesema kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli alilolitaka Mamlaka hiyo kuweka saini ya mwombaji na mtoaji wa vitambulisho hivyo.
“Tumeanza kutekeleza agizo la Mhe. Rais tangu mwezi Juni mwaka huu, hii inamaanisha kwamba vitambulisho vyote tulivyochapisha kuanzia mwezi Juni mpaka leo vina saini ya muombaji, saini ya mtoaji na tarehe ya kuzaliwa muombaji,” amesema Bi Rose.
Kaimu huyo amedai kuwa zoezi la ugawaji wa vitambulisho hivyo hivyo inasubiri kuzinduliwa na Rais Magufuli atakayekabidhiwa kitambulisho cha uraia namba moja na baadaye vitambulisho hivyo kugawiwa kwa wananchi wengine.
Bi Rose ameongeza kuwa Mamlaka hiyo itatumia taarifa za Tume ya Uchaguzi (NEC) zilizo katika vitambulisho vya kupigia kura na kuzihamishia katika kanzi data ya NIDA na mpaka sasa watanzania milioni 2.7 wamepatiwa vitambulisho hivyo na milioni 6.5 wamesajiliwa kwa ajili ya kupata vitambulisho hivyo.
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment