MAJERUHI USAIN BOLT AITWA KATIKA KIKOSI KITAKACHOENDA RIO


Mwanariadha Usain Bolt atatetea ubingwa wake wa Olimpiki wa mbio za mita 100, 200 pamoja na mbio za kupokezana vijiti baada ya kutajwa kwenye kikosi cha Jamaica kitakachoenda Rio.

Kulikuwa na hofu ya uwezekano wa Bolt kushiriki michuano hiyo ya Olimpiki nchini Brazil kutokana na kuwa na majeraha katika misuli yake ya mguuni, kiasi cha kushindwa kufanya majaribio ya kufuzu katika timu ya taifa.

Hata hivyo bingwa huyo mara sita wa michuano ya Olimpiki kwa mita 100 na 200 na ambaye anashikilia rekodi ya dunia ametajwa kwenye kikosi cha wachezaji 63 wa timu ya taifa ya Jamaica.
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment