Mtu mmoja ameripotiwa kupigwa risasi nje ya uwanja wa Ikulu ya Marekani baada ya kukaribia kituo cha ukaguzi na bunduki na kukataa amri ya kuishusha.
Taarifa zinasema mtu huyo alipelekwa hospitali akiwa katika hali mbaya, inasemekana alipigwa risasi baada ya kukataa amri iliyotolewa mara kadhaa ya kumtaka ashushe silaha aliyokuwa nayo.
Katika tukio hilo hakuna mwingine aliyedhurika, vyanzo vya habari kutoka Serikali ya Marekani vinasema maafisa wa usalama walikuwa wakimtazama mtuhumiwa na alikuwa hajaingia ndani ya Ikulu hiyo.
Mmoja wa Afisa wa Ikulu amesema Rais Barack Obama hakuwepo White House na alipewa taarifa ya hali hiyo kuwa kuna mtu aliyepigwa risasi amepelekwa hospitali yaGeorge Washngton University.
0 comments:
Post a Comment