Skendo ya wanajeshi wa JWTZ Congo, yazungumziwa na makao makuu



Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) chini ya Umoja wa Mataifa limekuwa likitekeleza majukumu ya ulinzi wa amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa takribani miaka mitatu. Siku kadhaa zilizopita ziliripotiwa taarifa za kulituhumu jeshi hilo kuhusika na unyanyasaji wa kijinsia unaodaiwa kufanywa kwa wananchi wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
April 08 2016 kutoka makao makuu ya Jeshi hilo wametoa taarifa za kusikitishwa na tuhuma hizo na hapa Afisa Habari wa Jeshi hilo James Macheta, ameyazungumza haya….>>>’Jeshi letu haliwezi kupuuza taarifa hizo, hivyo limeanza kuchukua hatua za kiuchunguzi ili kubaini ukweli wa tuhuma hizo ingawa rekodi za majukumu ya ulinzi wa amani zilizokwishafanywa na jeshi letu zinaonyesha hakukuwa na tuhuma kama hizo’;-James Macheta
>>>’Jeshi letu halitasita kuchukua hatua kali kwa wakaobainika katika tuhuma hizo, jeshi la ulinzi la wananchi wa Tanzania bado lipo imara na linaendelea kutekeleza majukumu yake nchini Congo kwa kufuata sheria na utaratibu wa Umoja wa Mataifa‘:-James Macheta
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment