Nay kuachia wimbo na video mpya, adai ni kali zaidi ya ‘Shika Adabu Yako’


Msanii wa muziki wa Hip Hop, Nay wa Mitego amesema anajipanga kuachia wimbo mpya ambao utapata nafasi ya kuchezwa katika vituo mbalimbali vya redio na TV nchini baada ya wimbo wake uliyopita ‘Shika Adabu Yako’ kutochezwa na vituo hivyo baada ya kudaiwa wimbo huo ulikiuka maadili. Nay akiwa kwenye maandalizi ya kazi mpya Nay akiwa kwenye maandalizi ya kazi mpya
Akizungumza na Bongo5 Jumatatu hii, Nay wa Mitego alisema wimbo huo utatoka pamoja na video mpya.

“Shika Adabu Yako, bado inafanya vizuri sana mtaani kusema kweli, lakini mimi ni msanii wa watu wote, kuna mashabiki wanahitaji kazi mpya. Kwa hiyo tarehe 9 mwezi wa 5 naachia wimbo mpya pamoja na video, na tarehe 6.6.16 nitachia wimbo mwingine video na Audio,” alisema Nay.
Aliongeza, “Huu ni ujio mpya wa Nay wa Mitego, ukiangalia ni tofauti na kazi zilizopita ambazo nilikuwa natoa audio na baadae video, lakini sasa hivi sitaki mchezo kila ngoma inatoka na video,”
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment