LIVERPOOL YAPAMBANA KIUME NA KUTINGA NUSUFAINALI LIGI YA UROPA

Timu ya Liverpool imepambana kiume ikitokea nyuma baada ya kufungwa na kutinga nusu fainali za Ligi ya Uropa kwa kuifunga Borussia Dortmund mabao 4-3 katika dimba la Anfield.

Katika mchezo huo Henrikh Mkhitaryan aliipatia Borussia Dortmund bao la kwa kwa shuti kali la karibu katika dakika ya tano, kabla ya Pierre Emerick-Aubameyang kuongeza la pili kwa kumalizia vizuri mpira katika eneo la penati.

Hata hivyo mwisho wa siku Dejan Lovren, Mamadou Sakho, Phillipe Coutinho pamoja na Divock Origi waliokoa jahazi la kocha Jurgen Klopp lisizame baada ya kupachika magoli na kufanya matokeo ya ujumla na mchezo wa mwanzo kuwa mabao 5-4.

Dejan Lovren akiruga juu angani na kupiga kichwa kiliozaa bao la nne la Liverpool katika ya dakika ya 90.
                    Pierre Emerick-Aubameyang akiruka sarakasi kushangilia goli lake
          Wachezaji wa Liverpool Origi na Sakho wakipiga selfie baada ya ushindi
Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment