MASHALI AKUBALI BWANA MDOGO TAMBA NI TISHIO HAPO BAADAYE


MASHALI

Pamoja na kufanikiwa kumshinda bondia Ibrahim Tamba, mkongwe Thomas Mashali amesema, bwan’mdogo huyo ni hatari.


Mashali amekubali kuwamba Tamba ni bondia bora ambaye atasumbua sana hapo baadaye.

Mashali alimshinda Tamba kwa pointi katika pambano lao la raundi 10 lililopigwa juzi kwenye Uwanja wa Ndani wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Pamoja na ushindi huo, Mashali alikiona cha moto ikiwa ni pamoja na kupasuliwa jicho na Tamba ambaye alikuwa akipambana bila kuchoka.



“Tamba ni bondia mgumu na alijiandaa sana, utaona nilifanya kila linalowezekana lakini aliendelea kupambana.
“Nimeshinda kihalali, kila mmoja ameona. Lakini lazima nikubali bwana mdogo alitoa upinzani mkali,” alisema.


Mashali amesema Tamba anaweza kuwa mmoja wa mabondia bora kabisa kama atajiendeleza vizuri katika mchezo huo.
P yhaa tv coming soon

Tuwe Pamoja Huku Ilikupata Stori ZOTE
share
 


face book ipyana stephen






  Share


















usisahau kusubscribe YouTube kwa kubonyeza hapa >>>Videos 





Share on Google Plus

About Unknown

Unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Email: Epyanastephene@gmail.com Phone:0719337774

0 comments:

Post a Comment